WAZIRI MKUU MAJALIWA: TANZANIA BADO INAHITAJI WAWEKEZAJI. AMTAKA BALOZI KIDATA KUTUMIA VIZURI FURSA YA UWEPO WAKE NCHINI KANADA KWA MANUFAA YA WATANZANIA
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa
(kulia), akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Canada, Balozi Alphayo
Kidata, ambaye alikwenda nyumbani kwake Majaliwa, Oysterbay
Jijini Dar es Salaam jana, kumuaga. (Picha zote na Ofisi ya Waziri Mkuu).
WAZIRI MAJALIWA:
TANZANIA BADO INAHITAJI WAWEKEZAJI. AMTAKA BALOZI KIDATA KUTUMIA VIZURI FURSA
YA UWEPO WAKE NCHINI KANADA KWA MANUFAA YA WATANZANIA.
NA MWANDISHI MAALUMU.
WAZIRI
MKUU KaWaziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini
Canada, Balozi Alphayo Kidata ambaye alikwenda kwenye Makazi ya Waziri
Mkuu Oysterbay jijini Dar es salaam kuaga, Mei 23, 2018. (Picha na
Ofisi ya Waziri Mkssim Majaliwa amesema Tanzania bado inahitaji wawekezaji na kupitia
kwenye uwekezaji, inapata fursa ya mitaji na teknolojia za kisasa.
Ayasema
hayo jana Jijini Dar es Salaam, wakati
akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Canada, Alfayo Kidata ambaye alikwenda
kumuaga nyumbani kwake.
Waziri
Mkuu alimtaka Balozi Kidata atumie fursa ya uwepo wake nchini Canada kuangalia
namna ya kuisadia nchi kuiimarisha katika sekta ya kilimo, madini na utalii.
“Tukiimarisha
sekta hizi, uchumi ndani ya nchi unakua, lakini pia tunategemea kutumia nchi
rafiki kukuza uchumi wetu wa ndani kwa maana ya kukuza mitaji na kupata
teknolojia za kisasa,” alisema.
mpango
wa Taifa wa maendeleo wa miaka mitano, lakini zaidi mkakati wetu wa kukuza
uchumi wa viwanda,” alisisitiza Waziri Mkuu.
Pia,
alimtaka Kidata kusimamia suala la upatikanaji wa masoko kwa ajili ya mazao
yanayozalishwa nchini ili wafanyabiashara na wakulima wa Tanzania waweze kuuza
bidhaa zao nje ya nchi.
“Hapa
nyumbani tuna mazao matano ambayo tumeazimia kuyafufua lakini masoko ya ndani
hayatoshi, kwa hiyo kazi yako mojawapo ukiwa huko ni kututafutia masoko,”
amesema.
Waziri
Mkuu alimweleza Balozi Kidata azingatie pia suala zima la kuongeza idadi ya
watalii. “Tunataka ukasaidie kutangaza nchi yetu ili watalii waje kuona vivutio
vyetu. Tunataka kuongeza idadi ya watalii kutoka milioni mbili ya sasa hadi
kufikia milioni tano ifikapo mwaka 2020,” alisema Majaliwa.
Aidha
Waziri Mkuu alimtaka Kidata akiwa huko afuatiilie fursa za masomo kwa ajili ya Watanzania
wanaotaka kusoma Canada na Cuba. “Nilipoongea na Makamu wa Rais wa Cuba,
aliahidi kuongeza idadi ya Watanzania wanaotaka kusomea udaktari. Kwa hiyo,
ukifika itabidi ufuatilie ahadi hiyo,” aliongeza kusema Waziri Mkuu.
Katika
hatua nyingine, Majaliwa alimsisitizia Balozi Kidata akifika Canada, awatambue
na kuwaunganisha Watanzania waishio nchini humo na awahamasishe wafanye kazi
ili waweze kuwekeza nyumbani.
Kwa
upande wake, akizungumza baada ya kuagana na Waziri Mkuu, Balozi
Kidata alisema atahakikisha anayafanyia kazi maelekezo
yote aliyopewa na Waziri Mkuu.
Alisema
anatambua kwamba Canada ina idadi ya watu zaidi ya milioni 40 na atafanya
juhudi zaidi za kuitangaza Tanzania ili waje kuona vivutio vilivyopo nchini.
Pia atafuatilia fursa za mafunzo kwa wanafunzi wa Kitanzania.
“Kwenye
suala la uchumi wa viwanda, tunahitaji kuwa na uzalishaji wa mazao ya kutosha.
Kwa hiyo tunahitaji kuwana kilimo cha uhakika na cha muda wote kuliko.
Tunahitaji kupata utaalamu na mitaji kwa ajili ya mashamba ya umwagiliaji,”
alisema.
Alisema
kuwepo kwa kilimo cha umwagiliaji, kutasaidia kuwe na uhakika wa upatikanaji wa
malighafi zitazakotumika kwenye viwanda.
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa (kulia), akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini
Canada, Balozi Alphayo Kidata.
No comments