WADAU WA SEKTA YA AFYA KUENDELEA KUBORESHA UTOAJI WA HUDUMA NCHINI.
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Mpoki Ulisubisya (Katikati), akisaini makubaliano ya malengo na vipaumbele vya kisera vya mwaka 2019/2020. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya TAMISEMI Dk. Zainab Chaula. Kulia ni Mwakilishi wa Wadau wa Maendeleo.
NA
WAJMW-DODOMA
SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto inaendelea kuboresha huduma afya nchini kwa kukarabati
vituo vya afya vipatavyo 350 ili utoaji
wa huduma za afya ya mama na mtoto hususani huduma za dharura wakati wa kujifungua.
Hayo yalisemwa jana Novemba 26, 2018 na Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, wakati wa mkutano wa mwaka wa
wadau wa sekta ya afya wa kujadilia njia zitakazowezesha kufikia malengo na
vipaumbele vya kisera vya mwaka 2019/2020 uliofanyika mapema jijini Dodoma.
“Sekta ya
afya tunaona inaendelea kupiga hatua kubwa sana katika maeneo mbalimbali
ikiwemo suala la kuimarisha miundombinu ambapo vituo vya Afya takribani 350
vimekarabatiwa kwa kuongeza miundombinu
kwa ajili ya kutoa huduma za afya za dharura ikiwemo huduma za kumtoa mtoto
tumboni,”alisema.
WAZIRI Ummy akihutubia kwenye mkutano huo jana
WAZIRI Ummy akihutubia kwenye mkutano huo jana
Waziri Ummy
alisema serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo duniani inahakikisha
sekta ya afya inapata mafanikio kwa kuboresha huduma nchini ikiwemo na kufikia
asilimia zaidi ya 90 ya dawa zinapatikana katika sehemu zote za kutoa huduma.
Aidha,
Waziri Ummy alisema mkutano huo ulikua na lengo la kukubaliana kutekeleza
vipaumbele nane (8) ambavyo serikali pamoja na wadau wa maendeleo itahakikisha
vinatekelezwa ipasavyo katika mwaka 2019/2020.
Maeneo hayo
ni pamoja na kuimarisha huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto ikiwa ni pamoja na kupunguza
vifo vitokanavyo na uzazi, kwa kuweka
miundombinu ya huduma za uzazi wa dharura na watoto wachanga kwani kwa
takribani hivi sasa watoto wachanga wapatao elfu 90 hufariki ndani ya siku 28
za mwanzo.
WADAU mabalimbali wa maendeleo wakifuatilia kwa makini majadiliano yaliyokua yanaendelea katika mkutano huo Jijini Dodoma jana.
WADAU mabalimbali wa maendeleo wakifuatilia kwa makini majadiliano yaliyokua yanaendelea katika mkutano huo Jijini Dodoma jana.
Eneo la pili
linahusu afya za wasichana na wavulana walio katika umri wa kubalehe ikiwa ni
pamoja na kutoa elimu ya kuepuka ngono katika umri mdogo na mimba
zisizotarajiwa.
Alitaja eneo
jingine ni kuongeza nguvu kazi katika sekata
ya afya ikiwa ni pamoja na kuajiri watumishi wa afya katika ngazi zote,
kuongeza ujuzi kwa kutoa nafasi za kusomesha watumishi ili kukidhi vigezo
vilivyoweka na shirika la afya duniani (WHO).
Kipaumbele
cha Nne, ni kuimarisha ubora wa huduma za afya utakaoenda sambamba na
uboreshaji wa miundombinu ya sehemu za kutolea huduma za afya za serikali
pamoja na kuongeza rasilimali fedha kwa ajili ya kutatua changamoto za afya kwa
kuongeza ya bajeti ya afya kutoka
kutoka Bilioni 31 hadi Bilioni 270 mwaka 2018/2019.
WKUGENZI mabalimbali wa maendeleo wakifuatilia kwa makini majadiliano yaliyokua yanaendelea katika mkutano huo.
WKUGENZI mabalimbali wa maendeleo wakifuatilia kwa makini majadiliano yaliyokua yanaendelea katika mkutano huo.
Naye Naibu
katibu Mkuu TAMISEMI anayeshughulikia afya Dk. Zainabu Chaula, alisema kwamba
wao kama sehemu ya utekelezaji wamejipanga kutekeleza maboresho ya afya ngazi
ya msingi kuanzia vijijini hadi Taifa kupitia sera ya afya.
Alisema wamejipanga
kuongeza kutoa elimu ya afya kwa umma kuanzia zahanati kwa kupanga mipango endelevu ili iende
sambamba kuanzia ngazi husika kwa kutumia kamati za afya kwenye vituo vya
kutolea huduma za afya nchini.
No comments